• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Wakulima wa tumbaku Mpanda Kati waezeka vyumba vya madarasa wilayani Tanganyika

Posted on: April 18th, 2017

Wakulima wa tumbaku Mpanda Kati wasaidia kuezeka vyumba vya madarasa Tanganyika.

Tanganyika. Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Bw. Salehe Mhando amekabidhiwa bandari 18 za mabati yenye urefu wa futi 10 ‘geji’ 28. Mabati hayo yametolewa na chama cha msingi cha wakulima wa tumbaku- Mpanda Kati kwa lengo la kuunga mkono juhudi za Mkuu wa wilaya ya Tanganyika anayehamasisha wananchi kujitolea kujenga vyumba vya madarasa kwa  kila shule.

 

“Msaada huu umeletwa wakati muafaka, nimeshahamasisha wananchi kujenga wenyewe vyumba vya madarasa na wameitikia kweli kweli.” Amesema Bw.Mhando.

Halmashauri ya wilaya ya Mpanda ina shule za msingi 52 na wanafunzi wa kuanzia darasa la awali hadi la saba 49,622. Vyumba vya madarasa vipo 320 na upungufu wa vyumba 839. Hadi sasa shule za msingi zina maboma mapya ya vyumba vya madarasa 96 na maboma ya ofisi 20.

Mkuu wa wilaya ametoa wito kwa wadau wa Elimu na wenye mapenzi mema kuendelea kuchangia michango ya ujenzi na ukamilishaji wa vyumba vya madarasa.

Maboma hayo 96 ya vyumba vya madarasa yatakapokamilika, kutabakia na upungufu wa vyumba vya madarasa 743 kwa upande wa shule za msingi kwa sasa. Wakati shule za sekondari zipo 9 tu katika halmashauri ya wilaya ya Mpanda. Shule 8 zinamilikiwa na halmashauri ya wilaya ya Mpanda wakati shule moja ni ya watu binafisi.

Halmashauri ya wilaya ya Mpanda ina kata 16 na kila kata inatakiwa iwe na shule ya sekondari ya kata. Ni kata 8 tu zenye shule za kata na hivyo bado halmashauri  inahitaji wadau wa Elimu na wengine kuunga mkono katika kuijenga Tanganyika mpya kielimu, uchumi na kimtazamo kwa ujumla.

Wakati huo huo, Mkuu wa wilaya ya Tanganyika amewashukuru bodi ya wakurugenzi wa chama cha msingi cha wakulima wa Mpanda Kati kwa kuwasaidia wananchi wa wilaya ya Tanganyika kwa kuwapa mabati. Hadi sasa yanahitajika mabati 4,512 katika halmashauri ya wilaya ya Mpanda.

Naye Meneja wa chama hicho cha wakulima wa tumbaku Mpanda Kati  Bw.Rajab Athuman amesema, “chama cha wakulima wa Mpanda Kati kimejikita kurejesha faida kwa wananchi wanaolima tumbaku kwa kusaidia upande wa Elimu kwa kuanzia”. Kwa muda wa miaka mitatu, chama kilijenga nyumba ya mwalimu katika shule ya msingi Mpembe, chumba cha darasa katika shule ya msingi Igalula na tarehe 18/04/2017 kilikabidhi bandari 18 za bati za kuezekea vyumba vya madarasa vilivyopo katika wilaya ya Tanganyika.

Hata hivyo, mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda Mhe. Hamadi Mapengo amekuwa mstari wa mbele kuhamasisha maendeleo ya wilaya ya Tanganyika katika nyanja mbali mbali.  Pia aliwashukuru wanachama na wafanyakazi wa chama cha wakulima wa tumbaku wa Mpanda Kati kwa msaada wa mabati ya kuezekea vyumba vya madarasa.

“Binafsi nimefanya kazi katika chama cha Mpanda Kati kwa muda wa miaka 9 nikiwa karani. Najua mchango wao kwa jamii, hasa halmashauri ya wilaya ya Mpanda (Tanganyika)”  , amesema Mheshimiwa Mapengo.

 

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • HALMASHAURI ZA WILAYA YA MOMBA NA MAKETE ZAKUTANA WILAYANI TANGANYIKA KUJIFUNZA BIASHARA YA KABONI.

    May 26, 2025
  • TANGANYIKA KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI KUBORESHA SUALA LA LISHE, WAKUU WA IDARA YA ELIMU NA WAKUU WA SHULE WAPEWA MBINU KUSIMAMIA UPATIKANAJI CHAKULA MASHULENI.

    May 13, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.