• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Upandaji wa miti Mwese

Posted on: December 7th, 2017

MKUU WA MKOA KATAVI AZINDUA UPANDAJI MITI-MWESE

Mkuu wa mkoa wa Katavi  Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga amewaongoza wananchi wa kata ya Mwese katika kuhamasisha upandaji wa miti mkoani Katavi ambapo zaidi ya miti 200 imepandwa katika eneo la kanisa. Zoezi hilo limefanyika  Disemea 7, 2017katika kata ya Mwese wilayani Tanganyika .

Wananchi wa Mwese wameitikia kwa wingi na zaidi ya miti 500,000 aina ya misindano (pinus patula) inatarajiwa kugawiwa bure kwa wananchi na taasisi mbali mbali kwa lengo la kupandwa na baadaye ije kuwanufaisha watu mbali mbali. Miti hiyo imefadhiliwa na shirika la kimataifa (THE NATURE CONSERVANCY)  kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Mpanda.

Licha ya The Nature Conservancy kufadhili shughuli  za uandaaji wa vitalu vya miche ya miti, mradi wa Tuungane umekuwa ukishirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Mpanda na wadau wengine ikiwa ni pamoja  na Tume ya Taifa ya mipango ya matumizi bora ya ardhi na wakala wa misitu Tanzania (TFS) katika uandaaji wa mipango ya matumizi bora ya ardhi vijijini na usimamizi wa pamoja wa raslimali za misitu katika wilaya ya Tanganyika.

 Mojawapo ya faida ya miti hiyo ni pamoja na kuongeza kipato kwa wananchi kwani mazao ya miti ni biashara. Mbao zinahitajika kwa wingi na kwa kuwa miti hiyo imegundulika kutoa mbao nyingi na nzuri.

Muhuga amesema, “wananchi wa mkoa wa Katavi mnapaswa kuchangamkia fursa zinazojitokeza. Eneo la Mwese kunastawi zao la kahawa, miti na migomba”.

Hata hivyo Muhuga ameongeza kuwa hakuna haja ya kuendelea kutegemea zao la tumbaku kama zao la biashara kwani limekuwa na changamoto ya kuwa na masharti magumu wakati kuna mazao mengine. Mazao mbadala wa tumbaku ni pamoja na kuanzisha mashamba ya miti ya kupandwa, pamba, alizeti, korosho na kahawa.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda mhe. Hamadi Mapengo aliwashukuru wadau wa utunzaji wa mazingira hasa shirika la Tuungane ambao wamekuwa wanashirikiana na Halmashauri katika utunzaji wa mazingira hasa matumizi bora ya ardhi.

Hata hivyo Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Bw. Romuli John amesema, “hata zao la chai linaweza kustawi katika maeneo ya Mwese. Tusiogope kujaribisha kupanda chai kama sehemu ya kujifunza”.

Hali ya hewa ya Mwese inakubaliana na mazao mbali mbali ya biashara bila kusahau matunda. Vyote hivyo vinaweza kukusababishia utajiri uliotukuka na kuwaacha watu wengine wakiwa midomo wazi.  Ndizi mbivu zinazopatikana Mpanda mjini, asilimia kubwa zinatoka Mwese.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • HALMASHAURI ZA WILAYA YA MOMBA NA MAKETE ZAKUTANA WILAYANI TANGANYIKA KUJIFUNZA BIASHARA YA KABONI.

    May 26, 2025
  • TANGANYIKA KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI KUBORESHA SUALA LA LISHE, WAKUU WA IDARA YA ELIMU NA WAKUU WA SHULE WAPEWA MBINU KUSIMAMIA UPATIKANAJI CHAKULA MASHULENI.

    May 13, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.