• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

TANGANYIKA YAWEKA MIKAKATI KUONGEZA VYANZO VYA MAPATO

Posted on: February 1st, 2023

HALMASHAURI YA TANGANYIKA YAWEKA MIKAKATI KUONGEZA VYANZO VYA MAPATO.


Halmashauri ya wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi katika kuongeza vyanzo vya mapato inakusudia katika bajeti ijayo kutenga fedha kwa ajili ya kujenga uwanja wa mpira ili kupitia mashindano mbalimbali halmashauri hiyo iweze kujiingizia mapato.


Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Tanganyika Shaban Juma, wakati akijibu hoja ya Diwani wa Kata ya Tongwe Frank Kibigasi katika kikao cha kawaida cha Baraza la madiwani aliyetaka kujua mikakati ya halmashauri katika kubuni chanzo cha mapato kupitia michezo na kusema kuwa tayari ameshampatia maelekezo Afisa Utamaduni kutafuta eneo kubwa kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa kisasa.


"Katika dunia ya leo sehemu nyingi masuala ya michezo wanayapa umuhimu ila sisi wilayani hapa hatuna kiwanja cha michezo. Tunaangalia eneo zuri ambalo linaweza kuwa kubwa na linafikika na watu kwa ukaribu ili tuweze kuingiza nguvu zetu"


Aidha, Diwani Kibigasi ameishauri halmashauri kuanzisha kituo cha kukusanyia ushuru eneo la Ngomalusambo kwa kuwa eneo hilo mazao yanapitishwa kiholela jambo linaloikosesha halmashauri mapato na kuinufaisha halmashauri nyingine.


Akichangia hoja hiyo, Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu amesema kipaumbele cha kwanza cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ni mapato hivyo halmashauri inapaswa kujipanga kutokana na mahitaji kuongezeka kila leo.


Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Tanganyika Hamad Mapengo amemtaka mkurugenzi kufanyia kazi ushauri uliotolewa na wajumbe wa Baralaza hilo ili kuleta ufanisi katika eneo la ukusanyaji mapato.


Katika hatua nyingine, Mapengo amewaomba Madiwani kuisaidia Serikali kuhimiza watoto waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza kuripoti haraka Shuleni.


"Turudi kwenye Kata zetu tuwahimize watendaji wa Vijiji. Mheshimiwa Rais ametoa fedha nyingi sana za kukamilisha miundombinu ya ujenzi wa madarasa,nyumba za walimu, tumepata fedha za madawati mmeona na Watumishi wanaendelea kufika kwa hiyo kazi yetu ni kuhakikisha tunahimiza wale watoto waende wakaripoti"


Katika shule ya Sekondari Majalila wanafunzi wapatao 27 bado hawajaripoti hadi sasa licha ya masomo kuanza jambo ambalo Mkuu wa wilaya ameagiza wanafunzi hao wabainishwe na wasakwe ili wakajiunge na masomo.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • HALMASHAURI ZA WILAYA YA MOMBA NA MAKETE ZAKUTANA WILAYANI TANGANYIKA KUJIFUNZA BIASHARA YA KABONI.

    May 26, 2025
  • TANGANYIKA KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI KUBORESHA SUALA LA LISHE, WAKUU WA IDARA YA ELIMU NA WAKUU WA SHULE WAPEWA MBINU KUSIMAMIA UPATIKANAJI CHAKULA MASHULENI.

    May 13, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.