• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Serikali kuhakiki upya ugawaji maeneo yenye Migogoro Katavi,RC aiomba tume kuharakisha utatuzi.

Posted on: October 13th, 2022

Pichani:Mwenyekiti wa Tume ya Mawaziri Nane ya Utatuzi wa Migogoro ya ardhi na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Mwashimba Ndaki akizungumza na Wananchi wa Kata ya Kasekese katika ziara yake kutatua migogoro ya Ardhi Mkoani Katavi.

Serikali imeridhia kufanya upya uhakiki wa ugawaji wa maeneo ambayo yameonekana kuwa na migogoro ya ardhi mkoani Katavi.

Akizungumza baada ya kutembelea baadhi ya maeneo hayo ikiwemo eneo la Visima Viwili lililopo katika Kata ya Kasekese wilayani Tanganyika,Mwenyeketi wa kamati ya mawaziri nane wa kisekta ambaye ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki ameelekeza kufanyika upya tathmini kwa maeneo yote Mkoani Katavi yenye migogoro ya mipaka baina ya Wananchi na Mamlaka za Uhifadhi ili kuja na suluhu ya kudumu ya kuondoa Migogoro hiyo

Aidha Mhe.Ndaki amewaomba Wananchi Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi  kuepuka kuendelea kufanya shughuli za  makazi katika maeneo ambayo hawana uhakika wa kuendelea kuishi kusudi kuepuka usumbufu na wakati mwingine hasara zisizokuwa na ulazima.

Awali akizungumza wakati wa utambulisho Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko aliiomba tume hiyo   ya Mawaziri Nane inayozunguka Nchi nzima   kutatua Migogoro mbalimbali ya ardhi kuharakisha utatuzi wa migogoro mbalimbali ya ardhi inayoendelea baina ya Wananchi na maeneo ya hifadhi Mkoani Katavi ili kutoa fursa kwa Wananchi kufanya maandalizi ya mashamba kwa wakati ili kuendana na msimu wa Mvua ambao umekaribia.

Kwa upande wao wananchi wameomba kamati hiyo kushughulikia kwa haraka jambo hilo ambalo limekuwa likisababisha migogoro inayojirudiarudia.

Kamati hiyo ya Wizara nane za kisekta imeundwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Kilimo na Ushirika, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais TAMISEMI na Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira)kwa ajili ya kutembelea maeneo yenye migogoro ya ardhi nchini na baadae kutoa mapendekezo ya namna ya kusuluhisha migogoro hiyo.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUWAJIBIKA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UMMA| DC BUSWELU AZINDUA MRADI WA RAIA MAKINI.

    July 25, 2025
  • MIRADI 106 YATEMBELEWA NA CMT| IMO YA AFYA & ELIMU| MAELEKEZO YATOLEWA KUKAMILISHA KWA WAKATI.

    July 22, 2025
  • KAMATI YA MWENGE MKOA YARIDHISHWA MAANDALIZI YA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU WILAYANI TANGANYIKA.

    July 16, 2025
  • DED TANGANYIKA AAGIZA UKAMILISHWAJI WA MIRADI| WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUUPOKEA MWENGE WA UHURU.

    July 11, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.