• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

RC MRINDOKO AKAGUA MRADI WA UJENZI WA MELI NNE BANDARI YA KAREMA, AWASIHI WANANCHI KURASMISHA ARDHI NA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MRADI.

Posted on: October 2nd, 2025

Tanganyika DC, Katavi – Oktoba 2, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Hoza Mrindoko, amefanya ziara ya kikazi katika Bandari ya Karema iliyopo Wilaya ya Tanganyika kwa ajili ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa meli nne za mizigo. Katika ziara hiyo, Mhe. Mrindoko ametoa maagizo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kuhakikisha maeneo ya kimkakati, ikiwemo Karema, yanapimwa na kurasimishwa kwa lengo la kuongeza thamani ya ardhi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa maeneo hayo.


Akiwa katika bandari hiyo ambayo tayari imeanza kutoa huduma mbalimbali, RC Mrindoko ameeleza kuwa kukamilika kwa meli hizo kutafungua fursa nyingi kwa wakulima na wafanyabiashara wa Mkoa wa Katavi na maeneo ya jirani kwa kurahisisha usafirishaji wa bidhaa mbalimbali na mazao kuelekea masoko ya kitaifa na kimataifa.

“Hii ni fursa ya kipekee kwa wananchi wa Katavi. Ni wakati sasa wa kuzalisha mazao ya kutosha kwa ajili ya masoko ya ndani na nje, kwa kuwa Bandari hii itakuwa lango la kibiashara litakalotuunganisha na masoko makubwa zaidi,” amesema RC Mrindoko.

Pia Katika kuhakikisha fursa hizo zinawanufaisha wananchi moja kwa moja, amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, Bw. Shabani Juma Juma, kuhakikisha upimaji na urasimishaji wa maeneo unatekelezwa kwa kasi.

“Namuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kuendeleza upimwaji wa ardhi katika maeneo haya na urasmishwaji wa maeneo haya ili kuyaongezea thamani, tusiachwe nyuma tuchangamkie fursa hizo.” RC Mrindoko.

Licha ya agizo hilo la Mkuu wa Mkoa wa Katavi, tayari Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika imekwisha aanza urasmishaji wa maeneo ya kimkakati ambapo timu ya wataalam kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika imeanza zoezi hilo kwa kupitia maeneo mbalimbali ikiwemo Kata ya Kasekese ambayo ni eneo moja wapo miongoni mwa maeneo yenye mzunguko mkubwa wa biashara na idadi kubwa ya makazi ya wananchi.


Kwa upande wake, Msimamizi wa Bandari ya Karema, Bw. Antony Poyo, anaeleza kuwa ujenzi wa meli hizo umefungua fursa za ajira kwa wakazi wa eneo hilo kupitia kazi za muda na ushiriki wa jamii katika huduma mbalimbali zinazohusiana na mradi.

Serikali kupitia taasisi husika inaendelea na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayolenga kuiunganisha Bandari ya Karema na maeneo mengine muhimu, ikiwemo ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mpanda hadi Karema pamoja na mpango wa kuunganisha bandari hiyo na reli ya kisasa ya SGR. Hatua hizi zote kwa pamoja zinatarajiwa kuifanya Bandari ya Karema kuwa kitovu cha usafirishaji, biashara na maendeleo ya kiuchumi kwa mkoa na taifa kwa ujumla.



Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DC ONESMO BUSWELU AKABIDHI MIFUKO YA SARUJI KUCHOCHEA UJENZI WA BWENI JIPYA LA WASICHANA SIBWESA SEKONDARI.

    October 08, 2025
  • WADAU NA WANANCHI WAASWA KUUNGANA PAMOJA UJEZI WA VITUO VYA MALEZI , MAKUZI NA MAENDELEO YA WATOTO HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA.

    October 04, 2025
  • RC MRINDOKO AKAGUA MRADI WA UJENZI WA MELI NNE BANDARI YA KAREMA, AWASIHI WANANCHI KURASMISHA ARDHI NA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MRADI.

    October 02, 2025
  • HII NDIO MIRADI NANE TANGANYIKA YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 2.5 ILIYO MKOSHA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA 2025.

    September 25, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.