• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Mkurugenzi afanya ziara ya Kutembelea Kata za Katuma na Mwese.

Posted on: April 27th, 2017

MKURUGENZI HALMASHAURI WILAYA YA MPANDA AONGEZA MILANGO YA MAWASILIANO KWA WATUMISHI.

Watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda wameagizwa kutoa taarifa ofisi ya Mkurugenzi mtendaji na kitengo cha habari za miradi na usimamizi wa shughuli  zinazoendelea katika maeneo ya kiutendaji.

Maagizo hayo yametolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda Bw. Romuli John Aprili 27, 2017 alipofanya ziara ya kujitambulisha kwa viongozi wa kata na kukagua miradi inayoendelea. Bw. John ameanza na kata za Katuma na Mwese ambapo aliongea na viongozi wa Kata na vijiji. “Lengo la ziara hii ni kutaka tufahamiane, kuelekezana na kusikiliza kero na ushauri….”. Alisema Mkurugenzi John.

Ziara ya kutembelea kata zingine 14 zilizobakia katika halmashauri ya wilaya ya Mpanda atapanga ratiba kuendana na upatikanaji wa muda. Jiografia ya maeneo ya wilaya ya Mpanda huwezi kufanya mikutano kwa zaidi ya kata mbili kwa siku. Mara baada ya kuteuliwa, alikutana na maandalizi ya kukimbiza mwenge kwa halmashauri ya wilaya ya Mpanda. Mwenge ulikimbizwa Aprili 3, 2017 na kuzindua miradi mbali mbali na mingine kuiwekea jiwe la msingi.

Hata hivyo Mkurugenzi John amesema kuwa amekuwa anapata taabu sana kuidhinisha malipo ya ujenzi wa miradi ambayo haijui imefikia hatua gani.  Kuanzia sasa anahitaji taarifa ya kila kitu kinachoendelea na siyo kuwa mgeni wa kila jambo au mradi. Wananchi ambao tunawategemea kushirikiana katika shughuli za maendeleo wamekuwa wakilalamikia mkanganyiko wa taarifa.

Lakini pia kuna maelekezo yanayotolewa kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa au Wilaya au Mwenyekiti wa halmashauri au Mkurugenzi kwenda kwa uongozi wa kata au kijiji na maagizo hayo yanakuwa yametolewa zaidi ya wiki 2 au 3 kwa wakuu wa Idara au Vitengo ili wayashushe kwa watendaji wa chini. Sasa kiongozi akienda kukagua utekelezaji wa maagizo anakutana na mshangao kutoka kwa viongozi wa kata au vijiji kwa kutokuwa na taarifa ya maagizo hayo.

Kila mtumishi wa halmashauri ameajiliwa na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji. Sasa itakuwa ajabu katika maeneo yako ya kiutawala ukutane na watu wanaoiba au kutorosha mali au mapato ya halmashauri ushindwe kutoa taarifa kwa Mkurugenzi Mtendaji  kwa kuhofia kuwa unaingilia majukumu ya watu wengine. Mawasilia ya uzalendo, ulinzi au kuzuia uovu hayahitaji kufuata mnyororo wa mawasiliano ya kiutumishi, kama una uhakika na ushahidi wasiliana na Mkurugenzi kwa namba ya simu ya mkononi.

Viongozi wetu wamekuwa na utaratibu wa kugawa namba za simu kwa wananchi ili kuondoa urasmu wa kuwapatia huduma wananchi. Watumishi wa serikali wameajiriwa kwa lengo la kuwahudumia wananchi na pale wananchi wanapoona hawatendewi haki au kupatiwa huduma ya ofisini, wana haki ya kumjulisha Mkurugenzi Mtendaji au hata Mkuu wa wilaya.

Serikali ya awamu ya tano (5) chini ya Mhe. Rais John Pombe Magufuli imejipanga kuwahudumia wananchi kwa kiwango cha juu. Shida iliyokuwepo kulikuwa hakuna mawasiliano ya moja kwa moja kati ya watumishi wa umma na wananchi. Pia kulikuwa na mkanyiko wa utoaji wa taarifa kutoka juu kwenda chini au chini kwenda juu.

Uongozi wa kata ya Mwese walimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda Bw. John kwa kuandaa ziara ya kuwatembelea viongozi hao. Waliongeza kwa kusema kuwa wamezoea kuwaona wakurugenzi kwenye ziara za kuambatana na Mkuu wa wilaya au Mkuu wa mkoa.

Bw. Romuli John aliteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda Disemba 19, 2016 baada ya aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji Bw. Ngalinda Hawamu kufariki Dunia Disemba 1, 2016. Marehemu Ngalinda aliteuliwa Juli 12, 2016 na kudumu kazini kwa cheo cha Ukurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda kwa muda wa miezi 5.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUWAJIBIKA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UMMA| DC BUSWELU AZINDUA MRADI WA RAIA MAKINI.

    July 25, 2025
  • MIRADI 106 YATEMBELEWA NA CMT| IMO YA AFYA & ELIMU| MAELEKEZO YATOLEWA KUKAMILISHA KWA WAKATI.

    July 22, 2025
  • KAMATI YA MWENGE MKOA YARIDHISHWA MAANDALIZI YA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU WILAYANI TANGANYIKA.

    July 16, 2025
  • DED TANGANYIKA AAGIZA UKAMILISHWAJI WA MIRADI| WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUUPOKEA MWENGE WA UHURU.

    July 11, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.