• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Madiwani Urambo wavutiwa na Biashara ya Hewa Ukaa Tanganyika DC.

Posted on: November 16th, 2022

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kutoka Mkoani Tabora wamefurahishwa kwa  namna ambavyo Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi  wamenufaika kupitia Mradi wa Uvunaji wa Hewa Ukaa katika Misitu inayomilikiwa na  Vijiji pamoja  na Halmashauri Wilayani humo

Timu ya Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo   ikijumuisha madiwani 24 pamoja na Wataalamu 10 wamefanya ziara Mkoani Katavi Wilayani Tanganyika 16 Novemba 2022 kwa lengo la  kujifunza namna ambavyo Halmashauri imetekeleza na kunufaika na Biashara ya hewa ukaa.

Akizungumza mara baada ya kutembelea kituo  cha kutolea huduma za Afya, katika Kijiji cha Kagunga,moja kati ya miradi inayotekelezwa kwa Fedha zitokanazo na uvunaji wa hewa ukaa Wilayani Tanganyika  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Bw.Adam Malunkwi amesema lengo la ziara hiyo ni kujifunza ili kutanua wigo wa kukusanyaji wa mapato.

“Tumefika hapa kwenu kwa maana ya kuja kujifunza,Ziara yetu imekuwa yenye  mafanikio  ya kutosha kwa sababu tumejionea kwa macho.Tumeshapewa darasa zuri sana kule Wilayani  tumefundishwa,tumeelewa na hapa tumejionea kwa macho namna ambavyo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika imenufaika kupitia Biashara ya Hewa Ukaa Hongereni sana. Kilichobaki hapa ni kutekeleza kwa vitendo kile ambacho tumejifunza ”Alisema Mwenyekiti Malunkwi.

Athmani Ali Mwinyiko mmoja wa Madiwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Urambo amesema ni muhimu kwa Wananchi Wilayani Tanganyika kuendelea kutunza misitu ili kuendelea kunufaika na Biashara ya Hewa Ukaa.

“Bahati nzuri wameanza  hatua ya chini na sasa wamepiga hatua kubwa. Kama Halmashauri imefanikiwa kupata zaidi ya Bilioni 4 kwa mwaka kupitia mradi mmoja wa hewa ukaa, ukijumlisha na miradi mingine maana yake mapato yatakua juu zaidi ukilinganisha na Halmashauri zingine ambazo hukusanya mapato chini ya Bilioni 1” alisema Diwani Mwinyiko.

Naye Diwani Kamende wa Viti Maalumu kutoka Tabora amesema wataitumia vyema elimu waliyoipata kuanzisha Biashara ya Hewa ukaa kwa kuwa Wilaya ya urambo imebarikiwa kuwa na Misitu ya kutosha.

“Wilaya ya Urambo tuna misitu mizuri lakini hatuifanyii kazi maana mnaweza mkawa na kitu lakini hamjui kukitumia,tumeona namna wanavyonufaika na Hewa ukaa na sisi niahidi tutaifanyia kazi Elimu hii na  tutawazidi hadi walimu”.Alisema Diwani huyo kutoka Uyombo huko Urambo.

Awali akiwasilisha mada ya mradi wa hewa ukaa  Mkuu wa Kitengo cha Maliasili Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Bw.Bruno Mwaisaka amewaambia Madiwani na Wataalamu kutoka Urambo kuwa ili waweze kunufaika na Biashara ya Hewa Ukaa ni muhimu kujipanga vyema kutunza Misitu pamoja na kuimarisha ulizi dhidi ya Wavamizi mbalimbali ikiwemo Majangili.

Ameongeza kuwa ni muhimu kuzingatia muongozo wa Kitaifa wa uanzishaji wa Biashara hiyo ya hewa ukaa na pia kuwa makini katika uandfaaji wa mikataba ya Biashara hiyo ili iweze kuleta manufaa zaidi kwao.

Biashara ya hewa ukaa Wilayani Tanganyika ilianza mwaka 2018 ukiendeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ,Taasisi ya CARBON Tanzania kwa kushirikiana na mradi wa Tuungane kwa Afya na Mazingira bora ukitekelezwa katika jumla ya Vijiji nane ambavyo ni Lugonesi,Mwese,Lwega,Bujombe,Kapanga,Katuma,Mpembe, na Kijiji cha Kagunga.

Aidha mradi huo unahusisha Misitu ya Vijiji yenye ukubwa wa Hekta 216,944 za Ardhi katika Vijiji vyote  ambapo  wakazi zaidi ya 34,242 wamefaidika na mradi katika sekta za Afya Elimu,na kuwezesha vikundi vya ujasiriamali.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KARATU WAFANYA ZIARA TANGANYIKA KUJINOA KUHUSU BIASHARA YA KABONI, MKURUGENZI NA MWENYEKITI WA HALMASHAURI WAAHIDI MAKUBWA.

    April 08, 2025
  • WANANCHI ZAIDI YA 3700 KUONDOKANA NA CHANGAMOTO YA MAJI SAFI NA SALAMA, TANGANYIKA.

    April 09, 2025
  • MIAKA MINNE YA RAIS DKT. SAMIA, TANGANYIKA YAPOKEA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 501 UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO.

    April 14, 2025
  • WATENDAJI WA KATA & VIONGOZI WA WAFUGAJI WAPIGWA MSASA MATUMIZI BORA YA ARDHI NA UFUGAJI WA KISASA KATIKA WILAYA YA TANGANYIKA

    March 27, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.