• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Karema yazidi kufanya vizuri matokeo kidato cha sita

Posted on: August 25th, 2017

Karema.Baraza la madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda limepongeza walimu na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Karema kwa kupata matokeo mazuri ya mtihani wa kidato cha sita 2017. Wanafunzi hao wa shule ya sekondari Karema wameongoza kwa mkoa wa Katavi kwa kushika nafasi ya kwanza kimkoa kati ya shule tatu na nafasi ya 50 kitaifa kati ya shule 449.

Pongezi hizo zimetolewa na diwani wa kata ya Karema mhe. Michael Kapata wakati wa mkutano wa baraza Julai 25, 2017 uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda(Idara ya maji).

“Mhe. Mwenyekiti shule ya Karema imetuweka katika ramani ya Tanzania. Mpaka sasa tunazidi kupokea wanafunzi waliopangiwa kuja kuanza kidato cha tano kwa wingi kutokana na matokeo mazuri tangu kuanzishwa kwa kidato cha tano na sita. Ni muda mwafaka wa Halmashauri kuwapongeza walimu na bodi ya shule ya Karema kama njia ya kuwashukuru”. Alisema mhe. Kapata.

Mhe. Kapata amekuwa msitari wa mbele kwa kuisemea shule hiyo ya sekondari ya Karema katika vikao vya waheshimiwa madiwani na kufuatilia maendeleo yake kwa karibu. Wanafunzi waliomaliza kidato cha sita katika sekondari ya Karema mwaka 2017 walikuwa 74 na wanafunzi 15 wamepata daraaja la kwanza( Division I), wanafunzi 50 daraja la pili (Divisioni II) na wanafunzi 9 wamepata daraja la tatu (Division II).

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Mhe. Hamad Mapengo ameahidi kuendelea kumkumbusha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda kuhakikisha anatekeleza ahadi zilizoahidiwa kwa wanafunzi waliohitimu kidato cha sita mwaka 2016. Wanafunzi hao walimwahidi mgeni rasmi kuwa watafanya vizuri katika mtihani wa kuhitimu kidato cha sita.

“Nikwambie tu Mkurugenzi, mwaka huu 2017 kama uongozi wa shule ungenialika kuwa mgeni rasmi katika shule ya sekondari Karema nisingekubali. Mwaka jana Halmashauri iliahidi kuwa kila mwanafunzi wa kidato cha sita atakayepata daraja la kwanza atapewa shilingi 50,000, daraja la pili 40,000 na daraja la tatu 30,000. Katika ahadi zilizotolewa, aliyetekeleza ni Mbunge wa Mpanda vijijini Mhe. Moshi Kakoso”. Alisema Mhe. Mapengo

Kwa matokeo ya kidato cha sita mwaka 2016, Karema ilikuwa nafasi ya 61 Kitaifa kati ya shule 423 na ya kwanza kwa mkoa wa Katavi kati ya shule 3. Wanafunzi 10 walipata daraja la kwanza, 46 daraja la pili na daraja la tatu wanafunzi 10.

Hata hivyo Mbunge wa jimbo la Mpanda vijijini Mhe. Kakoso aliwaasa madiwani kuhakikisha wanasimamia maendeleo ya wanafunzi kuanzia shule ya msingi hadi sekondari. Wanafunzi wanaofanya vizuri katika shule ya sekondari Karema katika matokeo ya kidato cha sita, asilimia kubwa wanatoka nje ya mkoa wa Katavi. Ni wajibu wa waheshimiwa madiwani kushirikiana na watalaam wa Halmashauri kuona namna ya wanafunzi wa ngazi ya chini nao wafanye vizuri katika mitihani yao ya kuhitimu kidato cha 4 na wao wapate nafasi za kujiunga kidato cha 5 na 6.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • HALMASHAURI ZA WILAYA YA MOMBA NA MAKETE ZAKUTANA WILAYANI TANGANYIKA KUJIFUNZA BIASHARA YA KABONI.

    May 26, 2025
  • TANGANYIKA KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI KUBORESHA SUALA LA LISHE, WAKUU WA IDARA YA ELIMU NA WAKUU WA SHULE WAPEWA MBINU KUSIMAMIA UPATIKANAJI CHAKULA MASHULENI.

    May 13, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.