• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Kambi JKT Tanganyika

Posted on: April 5th, 2017

JKT KUNUFAISHA WANANCHI WILAYANI TANGANYIKA .

Na Sylvanus Ntiyakenye.

Tanganyika. Halmashauri ya wilaya ya Mpanda imesaini hati ya kukabidhi eneo litakalojengwa kambi ya JKT katika wilaya ya Tanganyika. Makabidhiano hayo yamefanyika Aprili 5, 2017 katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda.

Eneo lililokabidhiwa lina ukubwa wa hekta 4,000 na  lipo Kaskazini mwa halmashauri ya wilaya ya Mpanda (Tanganyika). Eneo hili linapakana na msitu wa Tongwe Mashariki kwa upande wa Kaskazini, Mashariki linapakana na eneo la uwekezaji la halmashauri ya wilaya ya Mpanda. Kwa upande wa Kusini linapakana na barabara ya Mpanda –Kigoma na kijiji cha Vikonge, na Magharibi eneo limepakana na makazi ya Mishamo (kata ya Bulamata).

Mipaka ya eneo hili la JKT imeanzia karibu na eneo maarufu kwa jina la ‘Pembe la ng’ombe’ katika barabara ya Mpanda-Kigoma, mkono wa kulia kama unaelekea Kigoma jira namba 256899E, 9364061N. Mpaka unafuata barabara ya Mpanda-Kigoma kuelekea Kigoma kupitia jira namba 256692E, 9364270N hadi jira namba 256100E, 9365347N.

Pia mpaka unaelekea upande wa kusini kupitia jira namba 256041E, 9365310N hadi jira namba 254209E, 9360754N. Eneo linapita katika mpaka wa makazi ya Mishamo kuelekea upande wa Magharibi-Kaskazini kupitia jira namba 254454E, 9367050N hadi makutano ya mpaka wa msitu wa hifadhi wa Tongwe Mashariki jira namba 254859E, 9377488N.

Hata hivyo, kwa upande wa Kaskazini eneo la JKT litaishia kwenye mpaka wa msitu wa hifadhi wa Tongwe Mashariki unapoanzia na mpaka utapita katika jira namba 254944E, 9377262N, 255184E, 9376998N, 255544E, 9376782N,255712E, 9376734N, 255880E, 9376806N, 255976E, 9376398N, 255808E, 9375822N, 255832E, 9375462N, 256022E, 9375105N, 256239E, 9374165N, 256575E, 9373733N, 256671E, 9373158N, 256750E, 9372251N, 256894E.

Jira zingini ni namba 9371722N, 257302E, 9371098N, 257686E, 9370018N, 258358E, 9368747N,258598E, 9367954N, 258838E, 9367690N, 259222E, 9367402N, 259294E, 9367235N, 259390E, 9366827N hadi jira namba 259461E, 9366756N. Mpaka utaekea Kusini hadi jira namba 256899E, 9364061N mpaka ulipoanzia.

Faida watakazopata wananchi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda(Tanganyika) kutokana na JKT;

Mkuu wa jeshi la JKT Meja Jenerali Michael Isamuhyo amesema, “zipo faida nyingi ambazo wananchi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda watanufaika nazo”. Mojawapo ni kuimarisha ulinzi na usalama kwa mipaka ya halmashauri ya wilaya ya Mpanda.  Ulinzi ukiimalika, halmashauri itakusanya mapato yaliyokuwa yanatoroshwa na kwa njia za panya.

Pia Isamuhyo aliongeza kwa kusema, “JKT ina watalaam wa fani mbali mbali. Mfano walimua au madaktari watakuwa wanatoa huduma kwa vijiji vilivyo jirani na kambi hii kwa gharama za JKT”. Walimu wa JKT wataenda kufundisha wanafunzi wa halmashauri ya Mpanda kwa gharama za JKT. JKT itajenga kituo cha Afya katika kambi ila wananchi wa vijiji vinavyozunguka kambi hiyo watakuwa wanapata matibabu bure.

JKT watakuwa na mashamba darasa ya kilimo na mifugo, hivyo wananchi watapata fursa ya kujifunza kuendesha kilimo na ufugaji bila kuathili mazingira. JKT wataendesha kilimo cha umwagiliaji na kuwa walimu wazuri kwa wakazi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda.

Kwa kuwa tayari kuna kambi ya JKT, vijana wengi wa kutoka Tanganyika watapewa nafasi nyingi za kujiunga na jeshi hilo.

Naye Mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga amewapongeza JKT kwa kuanzisha kambi katika wilaya ya Tanganyika.  Kuwepo kwa kambi ya Jeshi, kutasaidia kuinua uchumi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda kwani zile mbao zilizokuwa zinatoroshwa kuelekea Uvinza, Kigoma ama Tabora zitaanza kulipiwa ushuru.” Mazao ya misitu yataanza kuwanufaisha wananchi wa wilaya ya Tanganyika”, alisema Muhuga.

Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda Mhe.Hamadi Mapengo ameshauri JKT kuwa na mahusiano mazuri na wananchi. Lengo la kuanzisha kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa katika wilaya ya Tanganyika liwe kweli kuinua uchumi wa wananchi wa wilaya ya Tanganyika, na siyo uwanja wa kupiga na kuwanynayasa wananchi wanaozunguka maeneo hayo. “Isifikie mahala ambapo sisi wawakilishi wa wananchi tunashindwa kuwafikia kambini kutokana na adhabu za kijeshi”, alisema Mhe. Mapengo

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) liliomba ardhi kwa halmashauri ya wilaya ya Mpanda kwa ajili ya uwekezaji katika kilimo na mifugo na ardhi ya kujenga kambi ya JKT. Vikao vya baraza la madiwani wa halmashauri vilipitisha azimio kuwa ardhi hiyo ikabidhiwe kwa JKT. Tayari ardhi hiyo imekabidhiwa kwa JKT mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga, Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Bw. Salehe Mhando, Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda Mhe. Hamadi Mapengo pamoja na Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda Bw.Romuli John na ujumbe wake.

Kwa upande wa JKT alikuwepo Mkurugenzi Mtendaji SUMA-JKT Brigedia Jenerali Charo Yateri na Mkuu wa JKT Meja Jenerali Michael Isamuhyo na ujumbe wake.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • HALMASHAURI ZA WILAYA YA MOMBA NA MAKETE ZAKUTANA WILAYANI TANGANYIKA KUJIFUNZA BIASHARA YA KABONI.

    May 26, 2025
  • TANGANYIKA KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI KUBORESHA SUALA LA LISHE, WAKUU WA IDARA YA ELIMU NA WAKUU WA SHULE WAPEWA MBINU KUSIMAMIA UPATIKANAJI CHAKULA MASHULENI.

    May 13, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.