• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

HII NDIO MIRADI NANE TANGANYIKA YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 2.5 ILIYO MKOSHA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA 2025.

Posted on: September 25th, 2025

HII NDIO MIRADI NANE ILIO ING'ARISHA WILAYA YA TANGANYIKA MBIO ZA MWENGE TAIFA 2025

Tanganyika, Katavi | Septemba 23, 2025 – Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko Hoza, ameongoza hafla ya makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru Kimkoa, ambapo Mwenge huo umepokelewa rasmi katika Wilaya ya Tanganyika na kukimbizwa umbali wa kilomita 166, ukitembelea na kuzindua jumla ya miradi 8 yenye thamani ya shilingi Bilioni 2,585,436,469/=.

MIRADI ILIOZINDULIWA WILAYA YA TANGANYIKA. 

Uzinduzi wa Mradi wa Maji Mazwe

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2025, Ismail Ali Ussi, amezindua Mradi wa Maji Mazwe uliogharimu Tsh Milioni 307.67. Mradi huu ni mkombozi mkubwa kwa wakazi wa Kijiji cha Mazwe, waliokuwa wakitembea zaidi ya kilomita 10 kufuata huduma ya maji safi na salama. Wananchi wameeleza kufurahishwa na mradi huo ambao unatarajiwa kumaliza kabisa adha hiyo ya muda mrefu.



Mapambano Dhidi ya Rushwa – Klabu ya Wanafunzi

Mwenge pia umezindua Klabu ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa katika Shule ya Msingi Luhafwe. Mradi huu umetajwa kuwa chachu katika kuimarisha uelewa wa watoto kuhusu madhara ya rushwa. Akizungumza wakati wa uzinduzi, Kiongozi wa Mbio za Mwenge alisema:

“Watoto wanapoanza kuelewa tangu wakiwa wadogo kuwa jambo fulani si sahihi, hujengewa msingi imara wa maadili. Nawasihi walimu na wazazi kuendelea kuwapa elimu ili wawe mabalozi wazuri wa mapambano dhidi ya rushwa.”


Lishe Bora kwa wanafunzi

Katika shule hiyo hiyo, Mwenge wa Uhuru umezindua Klabu ya Lishe inayolenga kuimarisha afya na lishe kwa wanafunzi. Takwimu za mkoa zinaonyesha mafanikio katika sekta hiyo ambapo hali bora ya lishe kwa watoto chini ya miaka mitano imeongezeka hadi 32.2% kutoka 38.4% mwaka 2015/2016.




Miradi Mingine 5 Iliyotembelewa na mwenge wa uhuru kitaifa:

Zahanati ya Kijiji cha Vikonge – inayolenga kuboresha huduma za afya kwa wakazi wa kijiji hicho.


Bweni la Wasichana – Shule ya Sekondari Majalila – kuinua mazingira ya kujifunzia kwa wasichana.



Ujenzi wa Barabara za Lami – Majalila – Inayolenga uboreshwaji wa miundombinu ya usafiri.


Mradi wa Kikundi cha Vijana “Bodaboda na Samia” – kusaidia ajira kwa vijana.


Uwekaji wa Jiwe la Msingi katika ujenzi wa Barabara ya Lami yenye urefu wa kilometa nne (4).


 

Pia Mwenge wa uhuru kitaifa katika kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita ya Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan juu ya matumizi ya nishati safi na salama iliongoza zoezi la ugawaji wa mitungi ya gesi ya kupikia kwa wakazi wa Kijiji cha vikonge, hii ni katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama nchini.

Miradi hii iliyo zinduliwa na mbio za mwenge wa uhuru kitaifa ni juhudi ya serikali ya awamu ya sita ya Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea maendeleo wananchi. 

Pamoja na hayo uongozi ofisi ya mkuu wa wilaya ya Tanganyika unawashukuru wananchi na wadau wote waliojitokeza kwa namna moja au nyengine wamechangia kukamilika kwa mbio hizo za mwenge wa uhuru kitaifa katika wilaya ya Tanganyika.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DC ONESMO BUSWELU AKABIDHI MIFUKO YA SARUJI KUCHOCHEA UJENZI WA BWENI JIPYA LA WASICHANA SIBWESA SEKONDARI.

    October 08, 2025
  • WADAU NA WANANCHI WAASWA KUUNGANA PAMOJA UJEZI WA VITUO VYA MALEZI , MAKUZI NA MAENDELEO YA WATOTO HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA.

    October 04, 2025
  • RC MRINDOKO AKAGUA MRADI WA UJENZI WA MELI NNE BANDARI YA KAREMA, AWASIHI WANANCHI KURASMISHA ARDHI NA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MRADI.

    October 02, 2025
  • HII NDIO MIRADI NANE TANGANYIKA YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 2.5 ILIYO MKOSHA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA 2025.

    September 25, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.