• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

DC ONESMO BUSWELU AKABIDHI MIFUKO YA SARUJI KUCHOCHEA UJENZI WA BWENI JIPYA LA WASICHANA SIBWESA SEKONDARI.

Posted on: October 8th, 2025

DC ONESMO BUSWELU AKABIDHI MIFUKO YA SARUJI KUCHOCHEA UJENZI WA BWENI JIPYA LA WASICHANA SIBWESA SEKONDARI.


Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Mhe. Onesmo Buswelu, amekabidhi mifuko ya saruji sita (6) kwa Shule ya Sekondari Sibwesa katika kuchochea ujenzi wa bweni la wasichana katika shule hiyo, bweni linalogharimu kiasi cha shilingi milioni 28.Hii ni katika kumwakilisha mdau wa maendeleo ya elimu, Bw. Peter Chilangazi kutoka Dodoma, ambaye ameguswa na juhudi za wananchi wa Kijiji cha Sibwesa waliochangia kiasi cha shilingi milioni 28 kwa ajili ya ujenzi wa bweni hilo jipya la wasichana katika Shule ya Sekondari Sibwesa.

Mdau huyo amevutiwa na juhudi za wananchi walizoonesha katika ujenzi wa mradi wa Shule Mpya ya Msingi Sibwesa, uliopo kwenye eneo la Shule ya Sekondari Sibwesa. Mradi huo unagharamiwa na fedha za Serikali Kuu (BOOST) kwa gharama za shilingi milioni 342. Mradi huo unategemewa kukamilika mwezi wa 12 mwaka huu na kuanza kazi rasmi Januari mwaka 2026.

Katika kuchochea hilo, Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Mhe. Onesmo Buswelu, amemuagiza Mtendaji wa Kijiji kutangaza kwa haraka sana tenda ya ujenzi wa bweni hilo la wasichana ili ujenzi uweze kuanza mara moja kwa manufaa ya wanafunzi wa kike waliopo shuleni hapo.

“Ukitoka hapa, nenda ukae kwenye mfumo. Kesha mpaka asubuhi uwe umeshatangaza tenda hiyo, sababu tumesha chelewa, na wanafunzi wa Sibwesa wanatakiwa kuanza kulala kwenye bweni jipya. Kwa sasa wanatumia darasa kama mbadala wa bweni. Hakuna kisingizio cha kucheleweshwa kwa kutangazwa kwa tenda hiyo,” amesema Mhe. Buswelu.

Sambamba na ziara hiyo ya kukabidhi mifuko ya saruji, Mheshimiwa DC Buswelu amekagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa shule mpya ya msingi Sibwesa, ujenzi unaohusisha majengo ya utawala, madarasa ya shule ya msingi na awali. Amemtaka mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi huo kwani unatakiwa kukamilika kwa wakati, mwezi wa kumi na mbili, ili uweze kutumika mwakani bila kuwepo kwa changamoto yoyote kwa wanafunzi.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA DISEMBA 5,2025 IMEENDESHA MAFUNZO YA UJAZAJI WA REJESTA ZA WAKAZI.

    December 05, 2025
  • EKARI 9 ZA BANGI ZATEKETEZWA, MKURUGENZI NA DC TANGANYIKA WATOA MAAGIZO

    December 03, 2025
  • DED TANGANYIKA DC ATAKA KASI UKAMILISHAJI WA MIRADI, ATOA MAELEKEZO KWA WATENDAJI

    November 27, 2025
  • MHE MHANDO APONGEZA KASI YA MAENDELEO TANGANYIKA DC, AHIMIZA AMANI NA UTULIVU

    November 27, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.