• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

DC BUSWELU ATANGAZA VITA NA WAZAZI WENYE WATOTO WASIORIPOTI SHULE

Posted on: February 14th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mheshimiwa Onesmo Buswelu ameuagiza uongozi wa kata ya Sibwesa wilayani humo kuhakikisha mpaka kufikia kesho wanafunzi wote zaidi ya 130 ambao walikuwa hawajaripoti shuleni wawe wameripoti shuleni,


Agizo hilo limetolewa leo wakati wa ziara ya kukagua hali ya wanafunzi kuripoti shuleni na kuhamasisha suala zima la lishe ili kuondokana na udumavu katika wilaya ya Tanganyika na Mkoa wa Katavi kwa ujumla,


Mheshimiwa Buswelu ameongeza kwa kuwataka wote wanaohusika na masuala ya elimu katika wilaya ya Tanganyika kuhakikisha wanaunda mpango mkakati utakaowawezesha wanafunzi wote ambao hawapo mashuleni wawe wameripoti shuleni kuendelea na masomo kama kawaida,


“Nakuagiza Afisa Tarafa shirikiana na Watendaji Kata na Vijiji na Serikali zote za Vijiji kuhakikisha wanafunzi hawa zaidi ya 130 mpaka kufikia siku ya kesho wawe tayari wameripoti kwenye shule zao” amesema DC Buswelu,


Katika hatua nyingine Mheshimiwa Buswelu ameutaka uongozi wa shule ya sekondari ya Sibwesa kuhakikisha wanafunzi wanaendelea kupata chakula shuleni hapo chakula ambacho kina mchanganyiko wa vyakula mbalimbali ili wanafunzi wasipatwe na tatizo la udumavu ambapo katika kusaidia hilo, Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ameshiriki zoezi la kupanda miti ya matunda aina ya mapera 20 na kutaka miti hiyo itunzwe ili wanafunzi wapate matunda shuleni hapo,



Vilevile, Mheshimiwa Buswelu ameahidi kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kuwatafutia Ng’ombe wa Maziwa ili wanafunzi hao waanze kupata uji wenye mchanganyiko na maziwa kuboresha afya zao,


Aidha, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Sibwesa Bi. Ernesta Chapuga amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika kwa kutenga muda wa kutembelea shuleni ambapo amemuahidi miti yote iliyopandwa leo itatunzwa ili iweze kuleta manufaa kwa wanafunzi waliopo na wale watakaokuja hapo baadae,


Mkoa wa Katavi licha ya kuwa kinara katika uzalishaji wa mazao ya chakula, bado hali ya udumavu kwa watoto iko kwa kiwango kikubwa hali iliyopelekea mkoa huo kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha unaondokana na tatizo hilo.


Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KARATU WAFANYA ZIARA TANGANYIKA KUJINOA KUHUSU BIASHARA YA KABONI, MKURUGENZI NA MWENYEKITI WA HALMASHAURI WAAHIDI MAKUBWA.

    April 08, 2025
  • WANANCHI ZAIDI YA 3700 KUONDOKANA NA CHANGAMOTO YA MAJI SAFI NA SALAMA, TANGANYIKA.

    April 09, 2025
  • MIAKA MINNE YA RAIS DKT. SAMIA, TANGANYIKA YAPOKEA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 501 UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO.

    April 14, 2025
  • WATENDAJI WA KATA & VIONGOZI WA WAFUGAJI WAPIGWA MSASA MATUMIZI BORA YA ARDHI NA UFUGAJI WA KISASA KATIKA WILAYA YA TANGANYIKA

    March 27, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.