• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Mkuu wa wilaya ya Tanganyika kuwalinda wanafunzi

Posted on: June 16th, 2017

Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Bw. Salehe Mhando ameahidi kuimarisha ulinzi kwa wanafunzi na watoto wote kwa ujumla. Mhando ameyasema hayo kwenye maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika ambayo kwa mkoa wa Katavi yamefanyikia Mishamo katika Halmashauri ya wilaya ya Mpanda. Wajibu wa wazazi ni kuhakikisha mtoto anatimiziwa mahitaji muhimu lakini suala la ulinzi ni la wazazi na serikali.

“Viongozi na watendaji wa serikali tuchukue hatua kwa wanaopuuzia suala la haki za watoto. Watoto wanalindwa kwa sheria ya mwaka 2009”. Alisema Mhando

Mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne mama Salma Kikwete alisema, “mtoto wa mwenzio ni mwanao”. Jamii ichukulie kuwa ina wajibu wa kuwalinda watoto wote kwa haki na usawa katika maeneo wanayoishi. Wazazi na walezi wameshauriwa kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola pindi wanapoona watoto wakitendewa vitendo visivyo vizuri.

Watu wengine wamefikia hatua ya kuwa na roho ya ukatili, mpaka wengine wanawabaka watoto wadogo na kuwasababishia maumivu na wengine kufariki Dunia. Wanaume wengine wanaoa watoto kwa kuwarubuni na kuwakatisha masomo. Sasa atakayesubutu kumpa mimba mwanafunzi ataenda jela miaka 30. Alisema Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Bw. Mhando

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Bw.Romuli John amewashauri wazazi na walimu washirikiane kubaini wanafunzi wanaotoka maeneo hatarishi ili waone namna ya kuwaimarishia ulinzi. Watoto walio chini ya miaka 10 wasiachwe peke yao kutembea umbali wa kilometa zaidi ya 6 tena unakuta wanaishi mashambani.

 Badala yake wanapaswa wale wanafunzi wenye umri mkubwa ndio waongozane na watoto wadogo. Watoto ambao wanatoka sehemu ambazo hazina wanafunzi wakubwa itabidi wazazi wawe wanawasindikiza watoto hao hadi shuleni na baadaye kuwafuata baada ya masomo.

Maeneo mengi katika Halmashauri ya wilaya ya Mpanda, nyumba ziko mbali sana na shule. Sasa ni vigumu mwanafunzi kurudi nyumbani kula chakula cha mchana na arudi tena shuleni kusoma ili kukamilisha ratiba ya masomo ya siku. Ndiyo maana uongozi wa shule na serikali waliwaagiza wazazi kuchangia chakula cha wanafunzi ili wawe wanakula shuleni.

Mtoto hawezi kufanya vizuri kimasomo kama muda mwingi anakuwa na njaa na bado akirudi nyumbani anakuwa hana uhakika na kupata chakula. Kibaya zaidi unakuta mtoto anakaa na watoto wenzake nyumbani huku wazazi wakiwa mashambani au kwenye shughuli za kibiashara.

Bw.John alikabidhi mipira ya miguu kwa shule 6 na mpira mmoja kwa Mtendaji wa kata ya Mishamo kwa lengo la kuhimiza mazoezi ili kujikinga na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Tanzania na nchi nyingine barani Afrika zinaungana kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika inayoadhimishwa kila Juni 16 kama ilivyoazimiwa na nchi wanachama 51 wa Umoja wa Afrika mnamo mwaka 1990.

Ikiwa siku hii ni siku kubwa barani Afrika, hivyo kila nchi mwanachama anatakiwa kuiadhimisha kulingana na makubaliano, hivyo kitaifa siku hii inaadhimishwa mkoani Dodoma  ikiwa na kaulimbiu isemayo, “Maendeleo Endelevu 2030: Imarisha Ulinzi Na Fursa Sawa Kwa Watoto.”

Ikumbukwe kuwa azimio hili lilipitishwa rami mwaka 1990 maalum kwa ajili ya kukumbuka mauaji ya watoto wa shule yaliyofanyika katika kitongoji cha Soweto, Afrika ya Kusini Juni 16, 1976 pale utawala wa Makaburu ulipowaua kikatili watoto waliokuwa wakidai haki ya kutokubaguliwa kutokana na rangi yao ambayo ni haki yao kimsingi wa haki za binadamu.

Ama kwa hakika kaulimbiu ya mtoto  wa Afrika ya mwaka huu imelenga kusisitiza juu ya uzingatiaji wa jukumu la ulinzi wa mtoto na utoaji wa haki sawa kwa watoto wote ili kufikia malengo endelevu ifikapo mwaka 2030.

Siku ya maadhimisho ya mtoto wa Afrika ni mahsusi kwa taifa na jamii kwa ujumla kutafuta changamoto, vikwazo na matatizo yanayomkabiri mtoto katika nyanja zote muhimu kama malezi, malazi, makazi, haki zake za msingi katika jamii na si tu kuadhimisha kama sherehe bali uwe ni uwanja wa kutatua shida zinazomkumba mtoto.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • HALMASHAURI ZA WILAYA YA MOMBA NA MAKETE ZAKUTANA WILAYANI TANGANYIKA KUJIFUNZA BIASHARA YA KABONI.

    May 26, 2025
  • TANGANYIKA KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI KUBORESHA SUALA LA LISHE, WAKUU WA IDARA YA ELIMU NA WAKUU WA SHULE WAPEWA MBINU KUSIMAMIA UPATIKANAJI CHAKULA MASHULENI.

    May 13, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.