• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Luhafwe kuwa mji wa kuigwa Tanzania

Posted on: June 22nd, 2017

Halmashauri ya wilaya ya Mpanda imerasmisha eneo la uwekezaji la Luhafwe na kupanga sehemu ya eneo kuwa mji wa biashara. Hayo yamesemwa Juni 22, 2017 na Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Bw. Salehe Mhando kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wanaoishi eneo hilo la Luhafwe.

Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mhando aliongozana na mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Mhe. Hamad Mapengo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Bw.Romuli John akiwa na watalaam wake.

Kabla ya kuanza mkutano, Afisa Mipango miji Bw. Elisha Mengele aliwapitisha wajumbe na viongozi wa eneo hilo na kuwaonesha mipaka ya eneo la makazi.

Eneo hilo la makazi lina ukubwa wa Hekta 2400 na tayari michoro mitatu yenye viwanja vya makazi 2164 imekamilika. Viwanja hivyo vitakuwa vya makazi tu na ukubwa umezingatia vipimo vya mjini na siyo mashamba.Pia huduma za kijamii nazo zimezingatiwa na kutengwa. Mfano shule, zahanati, maeneo ya wazi na huduma zingine za kibinadamu.

Aidha, Mkuu wa wilaya ya Tanganyika  Bw.Mhando amewaagiza wale wote wanaoishi katika maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za kilimo, Ufugaji au utalii wasitishe shughuli zao na kusubiria utaratibu watakaopangiwa na wataalam wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Mhe. Hamad Mapengo aliwashauri wakazi wa Luhafwe kukubaliana na utaratibu wa wataalam wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda.

“Huu ni mji na siyo kijiji wala kitongoji, tunahitaji kupaendesha kimji na kuzingatia mpango wa matumizi bora ya ardhi”. Alisema Mhe. Mapengo

Hata hivyo, Mhe. Mapengo aliwashauri wakazi wa Luhafwe wasiishi kwa mazoea kama zamani walipokuwa wanavamia maeneo na kujimilikisha mashamba makubwa bila utaratibu. Sasa utaratibu utaanza kufuatwa na wale watakao kiuka masharti na utaratibu, wakiondolewa kwa nguvu wasilalamikie viongozi.

Mpango wa matumizi wa Ardhi ya eneo la Uwekezaji (Luhafwe) umetekelezwa kwa mujibu wa sheria Na. 6 ya Matumizi ya Ardhi ya mwaka 2007, sheria ya Mipango miji Na. 8 ya mwaka 2007, sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999, sheria ya usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya Mwaka 2004, sheria ya Misitu Na. 14 ya mwaka 2002 na sheria ya maji Na. 1 ya mwaka 1999.

Lengo kuu la sheria hizi ni kuhifadhi Ardhi na Mazingira na kuyatumia katika namna ambayo ni endelevu kwa Matumizi ya vizazi vya sasa na vijavyo, kuongeza thamani ya Ardhi na tija katika uzalishaji mali na kuwa na Ardhi iliyopangiliwa katika utaratibu maalumu na kugawa kwa watu na wawekezaji kwa kuzingatia taratibu, kanuni na sheria.

Maeneo yaliyotengwa katika eneo la uwekezaji( Luhafwe) ni eneo la makazi lenye ukubwa wa Hekta 2400, eneo la viwanda Hekta 730, Utalii Ikolojia eneo la ukubwa wa Hekta 5036.Maeneo mengine yaliyotengwa ni eneo la kilimo wenyeji Hekta 4372, Kilimo uwekezaji Hekta 11,000 na malisho wenyeji Hekta 2000.

Hata hivyo kuna eneo lililotengwa kwa malisho ya mifugo uwekezaji Hekta 11,000 na benki ya ardhi Hekta 4,164.

Maeneo mengine ni uwekezaji wa jeshi la SUMA-JKT Hekta 3,000 na JKT kambi Hekta 1,000 na eneo lililiobakia la ukubwa wa hekta 1,298 ni msitu wa hifadhi. Eneo lote la uwekezaji la Luhafwe lina jumla ya ukubwa wa Hekta 46,000.

 

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • HALMASHAURI ZA WILAYA YA MOMBA NA MAKETE ZAKUTANA WILAYANI TANGANYIKA KUJIFUNZA BIASHARA YA KABONI.

    May 26, 2025
  • TANGANYIKA KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI KUBORESHA SUALA LA LISHE, WAKUU WA IDARA YA ELIMU NA WAKUU WA SHULE WAPEWA MBINU KUSIMAMIA UPATIKANAJI CHAKULA MASHULENI.

    May 13, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.